Francis Ogolla: Mwili wa Mkuu wa KDF Aliyeangamia Kwenye Ajali ya Helikopta Wawasili Nairobi - Tuko.co.ke
Francis Ogolla: Mwili wa Mkuu wa KDF Aliyeangamia Kwenye Ajali ya Helikopta Wawasili Nairobi

Francis Ogolla: Mwili wa Mkuu wa KDF Aliyeangamia Kwenye Ajali ya Helikopta Wawasili Nairobi

Mwili wa marehemu Mkuu Jenerali wa Jeshi la Ulinzi la Kenya (KDF) Francis Ogolla umepokelewa Nairobi.

Ogolla aliangamia na wenzake tisa baada ya chopa yao kuanguka Elgeyo Marakwet.

Rais William Ruto alithibitisha katika hotuba yake kwa taifa kwenye televisheni jioni ya Alhamisi, Aprili 18.

Ogolla alikuwa kwenye ndege ya Jeshi la Ulinzi la Kenya (KDF) iliyoanguka Keben kwenye mpaka wa Elgeyo Marakwet na kaunti za Pokoto Magharibi.

Katika kampuni yake kulikuwa na maafisa wengine tisa wa cheo cha kijeshi ambao pia walikufa katika ajali hiyo; wakaaji wawili walinusurika.

Viongozi waliofariki pamoja na Ogolla ni Brigedia Swale Saidi, Kanali Duncan Keittany, Luteni Kanali David Sawe, Meja George Benson Magondu, Kapteni Sora Mohamed, Kapteni Hillary Litali, Sajenti Mwandamizi John Kinyua Mureithi, Sajenti Cliphonce Omondi, na Sajenti Rose Nyawira.

Pia soma

Magazetini: Dakika za Mwisho za Mkuu wa Majeshi Francis Ogolla Kabla ya Ajali ya Helikopta

Read ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia news@tuko.co.ke au WhatsApp: 0732482690.

Chanzo: TUKO.co.ke

Online view pixel