Ureno 'ina na wasiwasi' kuhusu makubaliano ya kijeshi kati ya Sao Tome na Urusi
Serikali ya Ureno imeonyesha "wasiwasi mkubwa" baada ya kujua wiki hii kwamba Sao Tome na Principe, moja ya makoloni yake ya zamani barani Afrika, walitia saini makubaliano ya ushirikiano wa kijeshi na Urusi.
Imechapishwa:
"Mara tu makubaliano haya yalipojulikana, tulianza mashauriano na mamlaka ya Sao Tome," amesema Waziri wa Mambo ya Nje wa Ureno, Paulo Rangel, katika mahojiano yaliyotolewa Alhamisi jioni kwa televisheni ya SIC Noticias.
"Ureno kwanza, kisha nchi nyingine za Ulaya, zimeonyesha kushangazwa, wasiwasi na kufadhaika kwa makubaliano haya," amesema wakati akitambua kwamba Sao Tome ilikuwa nchi "huru" na ilikuwa na "uhalali kamili" wa kufanya uamuzi kama huo. Lakini, amesisitiza, "tunapojikuta katika hali ya kimataifa ambapo Shirikisho la Urusi linahusika na vita vya uchokozi ambavyo, zaidi ya hayo, vinahusisha bara la Ulaya, tumeelezea wazi wasiwasi wetu ".
Vyombo vya habari vya Ureno viliunga mkono kutoka Jumatano habari iliyoripotiwa na vyombo vya habari vya Urusi kulingana na ambayo Sao Tome na Urusi zilitia saini mnamo Aprili 24, huko Saint Petersburg, makubaliano ya ushirikiano wa kijeshi kutoa mafunzo au safari za ndege na meli za Urusi katika visiwa hivi katika Ghuba ya Guinea.
Haya yanajiri wakati rais wa Guinea-Bissau, koloni lingine la zamani la Ureno, alikuwa nchini Urusi kuhudhuria maadhimisho ya ushindi dhidi ya Ujerumani iliyokuwa chini ya utawla wa Kinazi.